• Breaking News

    USHAURI, ELIMU na TIBA YA ASILI +255 767-759-137

    Thursday 5 October 2017

    Katika ulimwengu huu wa mtandao matumizi ya laptop na simu yamekuwa ni muhimu sana na huwezi kuyatenganisha na shughuli zetu za kila siku. Lakini kwa bahati mbaya watu wengi wamekuwa wakivitumia vifaa hivi bila tahadhari ya afya ya uzazi.

    Utafiti uliofanyika na kuchapishwa na shirika la kimarekani ambao ulihusisha vijana 29 wenye umri miaka 26-45. Kila kijana alitoa shahawa ambazo ziligawanywa katika makundi 2. Kundi la kwanza liliwekwa mahali penye Wi-Fi ya laptop na kundi lingine lilitumika kulinganisha.

    TAZAMA VIDEO HAPA



    Lengo ilikuwa ni kupima athari ya Wi-Fi katika mwendo wa seli za uzazi (spamu), uwezo wa kuzalisha na athari katika vinasaba (DNA) vya seli hizo.

    Baada ya masaa 4 ilionekana kwamba ¼ ya mbegu zilizokuwa zimewekwa kwenye Wi-Fi hazikuwa na uwezo wa kuogelea (hazina uwezo wa kuzalisha).

    Mionzi ya ememe-usumaku (EMW) ya kama ya Wi-Fi na aina nyingine yoyote inaweza kuleta athari katika uzalishaji wa seli za uzazi kwa wanaume. Mamilioni ya seli za uzazi huzalishwa kila  siku katika korodani (kiwanda) na hivyo mionzi hii inapokuwa mingi na karibu na eneo hili kwa muda mrefu inapelekea vinasaba vya seli hizi kuathiriwa na kusababisha idadi ndogo sana ya seli hizi kutengeneza (low sperm count) au seli ambazo zitatengenezwa zinaweza kuwa na ulemavu kiasi kwa namna ya maumbo na utendaji kazi zisiweze kurutubisha.

    Tabia ya kupaka laptop mapajani wakati wa matumizi huleta joto katika korodani na hivyo kuathiri uzalishwaji wa mbegu za uzazi. Hii ni sanjari na kuoga maji ya moto kila siku, kuendesha vyombo vya moto kama pikipiki na magari kwa muda mrefu, kuvaa nguo zinazobana sana na tabia zingine zenye kusababisha joto katika korodani.

    Dr Wanyoike, mtaalamu wa afya ya uzazi anasema kumbukumbu zinaonesha kwamba tatizo la utasa kwa wanaume unaosababishwa na kuwa na mbegu kidogo limeongezeka sana hasa katika miaka ya hivi karibuni huenda ni kwa sababu ya matumizi yasiyo na tahadhari ya simu pamoja na kompyuta.

    Mwanaume anapomwaga inatakiwa kuwe na seli angalau milioni 20 ili kuweza kurutubisha yai lakini idadi ya watu wenye kiwango cha chini cha seli hizi inaongezeka kwa kasi.
    Shirika la afya la dunia, WHO linasema ndoa 1 kati ya 5 duniani sawa na 20% wanashida ya kupata mtoto (ugumba).

    Sababu nyingine zinazoweza kupelekea kuwa na idadi pungufu ya seli za uzazi ni;
    • ·      Uzito mkubwa na kiriba tumbo
    • ·      Matumizi ya madawa ya kulevya
    • ·      Uvutaji wa sigara- Hii huathiri mishipa ya damu
    • ·      Kuendesha baiskeli kwa muda mrefu mara kwa mara
    • ·      Kuendesha vyyombo vya moto kama pikipiki na magari makubwa kwa muda mrefu
    • ·      Kisukari
    • ·      Shinikizo la juu la damu

    Dr Nature anashauri, wanaume kuweka simu zao mbali na korodani. Kama ingelilazimu kukaa nayo ingewekwa mifuko ya shati/begi. Hii ni kinyume kwa wanawake ambao ni hatari kuweka simu karibu na maziwa kuepusha kansa ya matiti.

    Kama unatamani kuwa na mtoto panga mapema kwa kuwa na mtindo sahihi wa maisha. “Zaeni Mkaongezeke mkaijaze nchi” ni kauli ya Mungu aliyetuumba.

    Nature Clinic inakutakia uzao mwema!
    www.natureclinic.online


    [Kama umefurahia ujumbe huu, tafadhali shirikisha wenzako kadri iwezekanavyo tuokoe wenzetu wasiofahamu]

    No comments:

    Post a Comment